Kata swalah ya kujitolea na ujiunge na swalah ya faradhi

Swali: Nimeanza kuswali swalah ya kujitolea, kisha ikaanza swalah ya faradhi. Je, aikate swalah yake au aimalizie?

Jibu: Sunnah ni kwamba aikate swalah hiyo ili aelekee kuswali faradhi. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Ikikimiwa swalah, basi hakuna swalah isipokuwa ile ya faradhi.”

Ameipokea Muslim katika ”as-Swahiyh” yake.

Kwa hiyo ikianza swalah na yeye bado anaswali, basi aikate swalah hiyo na aingie pamoja na imamu ili ajitayarishe kuipata Takbiyr ya mwanzo.

Lakini ikiwa tayari ameshafanya Rukuu´ ya pili, basi hakuna kilichobaki. Ikiwa ataimalizia, swalah itakuwaimekwisha. Ikiwa yuko baada ya Rukuu´ ya pili au katika sijda ya mwisho, hakuna kinachomzuia kuimalizia, kwa sababu swalah hiyo tayari inakuwa imefikia mwisho.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1794/مشروعية-قطع-صلاة-النافلة-عند-اقامة-الصلاة-للفريضة
  • Imechapishwa: 03/07/2026