Swali: Tumesikia mara nyingi kwenye magazeti na majarida ibara inayosema “Kufanya upya utamkaji wa dini.” Nini maana ya ibara hii?

Jibu: Maana yake ni mbaya. Maana yake ni kwamba mtu asimwite kafiri kuwa ni kafiri (كافر) na badala yake amwite mtu au wenzetu (الآخر). Hivo ndivo wanavoona yabadilishwe matamko ya dini.  Watu wasisemi kafiri, mnafiki (منافق), zindiki (زِنْدِيق). Mtu anatakiwa kutamka matamshi ya jumlajumla kama vile kusema mtu. Huku ni kwa minajili ya kuwaficha wapotofu. Ni maana mbaya. Matamshi ya dini yametoka katika Qur-aan na Sunnah. Hayatakiwi kubadilishwa kabisa. Kuhusu njia zinazokwenda kinyume na Qur-aan na Sunnah zinatakiwa kubadilishwa na kupelekwa katika Qur-aan na Sunnah. Kwa sababu hizo ni kazi za watu.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Ma´aalim Manhaj Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah, uk. 41
  • Imechapishwa: 28/05/2021