Jiepushe na nyama za magharibi

Swali: Mimi sili nyama zinazotoka nje ya Saudi Arabia. Je, ni wasiwasi?

Jibu: Hapana, hili ni kwa ajili ya usalama. Nyama zinazotoka nje zinatia wasiwasi. Hawachinji kwa njia ya Kishari´ah. Wanachinja kwa mashine, kwenye kiwanda. Hawachinji wanyama kwa mujibu wa njia ya Kishari´ah. Wana makampuni na viwanda vyao. Wanachinja kwa mashine. Wanaua ndege kwenye maji ya moto sana na mfano wa hayo. Hawawezi kuchinja kila kuku, njiwa au mnyama mwingine. Ni vigumu kwao kufanya hivo. Wanachinja kwa mashine hizi. Ndio maana lililo salama zaidi ni kujiepusha na nyama hizi. Vinginevyo vichinjwa vya Ahl-ul-Kitaab ni halali lau watachinja kwa njia ya Kishari´ah.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (34) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/ighastah%20-%201%20-%202%20-%201436.mp3
  • Imechapishwa: 17/06/2015