Swali: Baadhi ya watu unapowakataza basi ndio huzidisha. Kwa mfano ameweka kubwa anapaza sauti zaidi, kama anavuta sigara anakupulizia usoni mwako.

Jibu: Mwombee uongofu. Kuna watu ambao ni wapumbavu na kuwakataza hakuwazidishii jengine isipokuwa shari zaidi. Lakini muumini anapaswa awe mwenye akili zaidi kuliko yeye, awe mpole na mwenye subira. Amwambie:

الله يهديك

”Allaah akuongoze.”

الله يعيذك من الشيطان

”Allaah akulinde na shaytwaan.”

Anatakiwa awe mbora kuliko yeye.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24620/بم-ينصح-من-يتعرض-للاذى-عند-انكار-المنكر
  • Imechapishwa: 14/11/2024