Swali: Ni ipi hukumu ya Udhhiyah? Je, anapata dhambi mwenye kuacha kama ana uwezo?
Jibu: Hukumu ya Udhhiyah ni kwamba ni Sunnah kwa mwenye uwezo na sio lazima. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akichinja kondoo wawili wenye kunona. Maswahabah pia walikuwa wakichinja katika uhai wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na baada ya kuaga kwake dunia. Vivyo hivyo waislamu baada yao. Haikupokelewa kwa mujibu wa dalili za Kishari´ah yanayofahamisha juu ya kwamba ni lazima. Maoni yanayosema kuwa ni lazima ni dhaifu.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (18/36)
- Imechapishwa: 06/06/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket