I´tikaaf ndani ya chumba cha mlinzi na chumba cha kamati ya zakaah

Swali: Je, chumba cha mlinzi na chumba cha kamati ya zakaah ndani ya msikiti vinazingatiwa ni sawa kukaa I´tikaaf ndani yavyo pamoja na kuzingatia kwamba milango ya vyumba hivi viko ndani ya msikiti?

Jibu: Vyumba vilivyoko ndani ya msikiti na milango yake ambayo inafunguliwa kwa ndani ya msikiti vinayo hukumu ya msikiti. Lakini vikiwa nje ya msikiti sio sehemu katika msikiti hata kama milango yake itakuwa ndani ya msikiti.

´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz

´Abdur-Razzaaq ´Afiyfiy

´Abdullaah bin Qu´uud

  • Mhusika: al-Lajnah ad-Daaimah
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: al-Lajnah ad-Daaimah (10/412)
  • Imechapishwa: 25/04/2022