Swali: Nilisafiri kutoka Jeddah kwenda ar-Riyaadh kisha nikarudi siku hiyohiyo. Nilifika Jeddah wakati wa swalah ya ´Aswr. Je, inafaa kwangu kufuta juu ya soksi pamoja na kwamba nia yangu ilikuwa kwa ajili ya safari?

Jibu: Ikiwa muda haujatimia hapana utatizi wowote kwamba inafaa kufuta. Ni mamoja uko katika hali ya safari au ya ukazi. Ama ikiwa muda umekwishatimia basi atatakiwa kuvua khofu zake, atawadhe na aoshe miguu yake.

  • Mhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: I´laam-ul-Musaafiriyn, uk. 27
  • Imechapishwa: 27/04/2020