Swali: Ilikuwaje swalah ya Manabii kabla ya Uislamu na ilikuwaje swalah ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) na Maswahabah wake kabla ya safari ya usiku na safari ya kupandishwa juu mbinguni?

Jibu: Swalah ya Manabii Allaah ndiye Mjuzi zaidi nayo. Sisi tumeamrishwa kuswali swalah tuliyoamrishwa na Nabii wetu Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam). Kwa hiyo ni juu yetu kuswali kama alivyokuwa akiswali (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam). Amesema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam):

“Swalini kama mlivyoniona nikiswali.”

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (29/240)
  • Imechapishwa: 01/03/2026