Iko wapi dalili yako, ee al-Khaliyliy?

Ni upi ushahidi wa al-Khaliyliy kwamba watu wa madhambi makubwa watadumu milele Motoni? Hali ya kuwa Allaah anasema:

إِنَّ اللَّـهَ لَا يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَاءُ

“Hakika Allaah hasamehi kushirikishwa, lakini anasamehe yaliyo chini ya hayo kwa amtakae.”[1]?

al-Bukhaariy amepokea katika ”as-Swahiyh” yake kupitia kwa Abu Dharr ambaye ameeleza:

“Yeyote atakayekufa juu ya upwekeshaji ataingia Peponi hata kama atazini na  kuiba” Alikariri hivo mara tatu.”[2]

Imekuja katika “Swahiyh Abiy Daawuud” ya kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Uombezi wangu kwa ajili ya watu wa madhambi makubwa kutoka katika ummah wangu.”[3]

Utafiti wa mada hii utakuja wakati wa kujadili dai lake ”kuhusu kudumu kwa watu wa madhambi makubwa Motoni” katika juzu ya tatu ya kitabu hiki.

[1] 4:48

[2] al-Bukhaariy (123).

[3] Abu Daawuud (4/625), na. 2435.

  • Muhusika: ´Allaamah ´Aliy bin Naaswir al-Faqiyhiy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ar-Radd al-Qawiym, uk. 266-267
  • Imechapishwa: 11/09/2026