Hakuna, si katika Qur-aan wala Sunnah, yanayohalalisha makundi na vyamavyama. Bali yaliyomo kwenye Qur-aan na Sunnah ni kusemwa vibaya kwa jambo hilo. Amesema (Ta´ala):
فَتَقَطَّعُوا أَمْرَهُم بَيْنَهُمْ زُبُرًا ۖ كُلُّ حِزْبٍ بِمَا لَدَيْهِمْ فَرِحُونَ
”Lakini wakalivunja jambo lao baina yao makundi mbalimbali, kila kundi kwa waliyokuwa nayo linafurahia.”[1]
Hapana shaka kwamba vyamavyama hivi vinapingana na yale aliyoamrisha Allaah. Bali yale aliyosisitiza pindi aliposema (Ta´ala):
إِنَّ هَـٰذِهِ أُمَّتُكُمْ أُمَّةً وَاحِدَةً وَأَنَا رَبُّكُمْ فَاعْبُدُونِ
“Hakika huu ummah wenu ni ummah mmoja; Nami ni Mola wenu, hivyo basi niabuduni.”[2]
[1] 23:52-53
[2] 21:92
- Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Fataawaa ´Ulamaa-ul-Kibaar fiy al-Irhaab wat-Tadmiyr, uk. 408
- Imechapishwa: 18/01/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)