Ibn Baaz ndoa ya mwanadamu na jini

Swali: Je, imepokelewa kuoana kati ya wanadamu na majini?

Jibu: Haijapokelewa. Hatujui jambo lolote kuhusu hilo. Katika hilo kuna mitazamo tofauti kwa wanazuoni, kwa sababu jambo hilo halijulikani. Haiwezekani kuthibitisha Uislamu wao wala dini yao. Kwa hiyo haifai kuoana nao kabisa, kwa sababu hatuwezi kujua ukweli na kama madai yake ya Uislamu ni ya kweli au si ya kweli. Hivyo jambo hilo liko katika khatari.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1911/حكم-الزواج-من-الجن-او-تزويجهم
  • Imechapishwa: 28/12/2025