Ibn Baaz kupeana mikono baada ya swalah

Swali: Baadhi ya watu wanatoa salamu kuliani na kushotoni wanapomaliza swalah na baadhi yao wanasema kuwa ni jambo la heshima na kuongeza kheri kwa salamu baina ya waislamu na hakuna tatizo. Je, hili ni sahihi?

Jibu: Hili likiwa wanapokutana katika safu na baadhi yao wakapeana salamu baada ya kumaliza swalah ya Sunnah na wakasalimia na kupeana mikono, hili ni jambo zuri. Ama baada ya swalah ya faradhi hapana, kwa sababu hili halina msingi. Ama katika swalah za Sunnah na ´ibaadah nyingine za kujitolea. Swalah ya Sunnah, yote haya ni mazuri.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1070/حكم-مصافحة-المصلين-بعد-الفريضة
  • Imechapishwa: 24/01/2026