Ibn Baaz kuhusu kumzika maiti ndani ya sanduku

Swali: Maiti akiwa ndani ya sanduku wakati mwingine kwa dharurah, kama alikuwa amezama majini au mwili wake unanuka sana?

Jibu: Akizama majini na akahamishwa kutoka nchi moja kwenda nyingine, hakuna kosa kumzika katika kaburi akiwa ndani ya sanduku.

Swali: Je, azikwe kaburini pamoja na sanduku?

Jibu: Ikiwa kunakhofiwa kutokana naye, basi asitolewe ikiwa kunaleta madhara. Lau akitolewa vilevile hapana vibaya. Lakini kama hakuna madhara, atatolewa kutoka kwenye sanduku na kuwekwa ndani ya mwanandani. Lakini ikiwa kutoa mwili wake kutawasumbua watu kwa sababu ya harufu au kuleta madhara, basi huzikwa akiwa ndani ya sanduku na hilo linatosha.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1154/حكم-وضع-الميت-في-تابوت-داخل-القبر
  • Imechapishwa: 31/01/2026