Ibn Baaz kuhusu kumswalia maiti aliyekufa mji mwingine

Watu wametofautiana kuhusu hili: je, kila maiti aliyekufa mji wa mbali anaswaliwa, haswaliwi au ni jambo linahitaji upambanuzi? Lililo na nguvu zaidi ni la tatu. Msingi ni kutofanya umaalum. Kauli ya yule mwenye kusema kwamba hakuna yeyote aliyemswalia an-Najaashiy katika nchi yake iko mbali sana. Bali alikuwa na wafuasi waliomswalia na jamaa zake. Lililo na nguvu zaidi ni kwamba anatakiwa kuswaliwa yule mwenye mchango na kutangulia katika Uislamu, kama mfano wa an-Najaashiy.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ibn Baaz, uk. 109
  • Imechapishwa: 23/05/2025
  • Mkusanyaji: Shaykh Abiy Muhammad ´Abdullaah bin Maaniy´