Swali: Ni nini makusudio ya Hadiyth isemayo:
”Muumini mwenye nguvu ni bora na mwenye kupendwa zaidi na Allaah kuliko muumini dhaifu.”?[1]
Kuna wanaosema kuwa makusudio ya nguvu ni za mwili.
Jibu: Hapana, haikusudiwi nguvu ya mwili pekee. Nguvu inayokusudiwa hapa ni nguvu ya matendo. Akiwa na nguvu zaidi ya ndovu, lakini haamrishi mema wala hakatazi maovu, basi hawezi kuitwa kuwa ni mwenye nguvu; badala yake anakuwa ni dhaifu, hata kama ana nguvu zaidi kuliko ndovu.
[1] Muslim (04/2052).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/25244/ما-المقصود-بحديث-المومن-القوي-خير-واحب-الى-الله
- Imechapishwa: 20/02/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)