Swali: Vipi kuhusu kusujudia sanamu?
Jibu: Kusujudu kwa sanamu ni ukafiri mkubwa, ni mamoja iwe kwa ajili ya sanamu, aliye ndani ya kaburi, kwa mtawala, kwa Zayd au kwa ´Amr. Kusujudia asiyekuwa Allaah ni ukafiri mkubwa. Allaah amesema:
فَاسْجُدُوا لِلَّـهِ وَاعْبُدُوا
”Basi msujuduni kwa ajili ya Allaah na mwabuduni Yeye.”[1]
Swali: Wako wanaosema kuwa ni lazima uitakidi?
Jibu: Hapana, hapana. Pale tu atapomsujudia asiyekuwa Allaah anakufuru.
Swali: Wamelinganisha na sujuud ya Mu´aadh kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?
Jibu: Hapana, hapana. Sujuud ya Mu´aadh Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwonya kwamba hakuna yeyote anayepaswa kumsujudia mwingine na akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Lau ningemwamrisha mtu kumsujudia yeyote, basi ningemwamrisha mwanamke amsujudie mumewe, kutokana na ukubwa wa haki yake juu yake.”[2]
Kuhusu sujuud ya ndugu zake Yuusuf, hilo lilikuwa katika Shari´ah ya waliokuwa kabla yetu. Kwao wao ilikuwa ni sujuud ya mamkizi. Kadhalika sujuud ya Malaika kwa Aadam ni sujuud ya heshima na mamkizi. Hilo ni jambo maalum. Inapokuja katika Shari´ah hakuna jambo la kumsujudia yeyote asiyekuwa Allaah:
فَاسْجُدُوا لِلَّـهِ وَاعْبُدُوا
”Basi msujuduni kwa ajili ya Allaah na mwabuduni Yeye.”
[1] 53:62
[2] at-Tirmidhiy (1159).
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/29286/حكم-السجود-لغير-الله-تعالى
- Imechapishwa: 04/09/2025
Swali: Vipi kuhusu kusujudia sanamu?
Jibu: Kusujudu kwa sanamu ni ukafiri mkubwa, ni mamoja iwe kwa ajili ya sanamu, aliye ndani ya kaburi, kwa mtawala, kwa Zayd au kwa ´Amr. Kusujudia asiyekuwa Allaah ni ukafiri mkubwa. Allaah amesema:
فَاسْجُدُوا لِلَّـهِ وَاعْبُدُوا
”Basi msujuduni kwa ajili ya Allaah na mwabuduni Yeye.”[1]
Swali: Wako wanaosema kuwa ni lazima uitakidi?
Jibu: Hapana, hapana. Pale tu atapomsujudia asiyekuwa Allaah anakufuru.
Swali: Wamelinganisha na sujuud ya Mu´aadh kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)?
Jibu: Hapana, hapana. Sujuud ya Mu´aadh Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alimwonya kwamba hakuna yeyote anayepaswa kumsujudia mwingine na akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Lau ningemwamrisha mtu kumsujudia yeyote, basi ningemwamrisha mwanamke amsujudie mumewe, kutokana na ukubwa wa haki yake juu yake.”[2]
Kuhusu sujuud ya ndugu zake Yuusuf, hilo lilikuwa katika Shari´ah ya waliokuwa kabla yetu. Kwao wao ilikuwa ni sujuud ya mamkizi. Kadhalika sujuud ya Malaika kwa Aadam ni sujuud ya heshima na mamkizi. Hilo ni jambo maalum. Inapokuja katika Shari´ah hakuna jambo la kumsujudia yeyote asiyekuwa Allaah:
فَاسْجُدُوا لِلَّـهِ وَاعْبُدُوا
”Basi msujuduni kwa ajili ya Allaah na mwabuduni Yeye.”
[1] 53:62
[2] at-Tirmidhiy (1159).
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/29286/حكم-السجود-لغير-الله-تعالى
Imechapishwa: 04/09/2025
https://firqatunnajia.com/hukumu-ya-kumsujudia-asiyekuwa-allaah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
