Swali: Akiapa huku akiwa na dhana kubwa ya kuwa jambo fulani limetokea, lakini halijatokea. Je, atalazimika kutoa kafara?
Ibn Baaz: Kwa maana ya kwamba ameapa kwamba jambo hilo limetokea?
Muulizaji: Ameapa kwamba jambo fulani limetokea, lakini halijatokea.
Ibn Baaz: Amesahau?
Mwanafunzi: Dhana kubwa imempelekea kufanya hivo.
Ibn Baaz: Naapa kwamba fulani amekuja, naapa kwamba fulani amefika na naapa kwamba mwezi umeshaingia. Akifikiri hivo?
Mwanafunzi: Ndiyo.
Jibu: Sahihi ni kwamba hakuna juu yake kafara, kwa sababu anajiona ni mwenye kusema ukweli.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/28966/حكم-من-حلف-على-شيء-بغلبة-ظنه
- Imechapishwa: 14/05/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket