Hizb-ut-Tahriyr ni pote khabithi. Pengine mkaonelea kuwa ni maneno makubwa kusema ya kwamba ni khabithi mwanzoni wa maneno yangu. Nilitakiwa kuwapa utangulizi kwanza. Ni pote khabithi. Limeundwa Jordan na linatokamana na al-Ikhwaan al-Muslimuun. Waliliandikia lirudi, lakini likakataa. Kiongozi wake alikuwa Taqiyy-ud-Diyn an-Nabhaaniy.

Inapokuja katika ´Aqiydah, wanasema kuwa hawachukui isipokuwa kutoka kwenye akili tu. Na ikitajwa katika Qur-aan na Sunnah, basi ni lazima iwe Mutlaq. Kutokana na hilo wanakanusha adhabu ya kaburi na kujitokeza kwa ad-Dajjaal. Kuhusu wahusika hawajali kufundisha tabia au elimu. Ni pote linaloshaji´isha wafuasi wake kujishughulisha tu na siasa inayoenda kinyume na dini. Kiongozi wake aliulizwa ni kwa nini pote lake halina masomo ya Qur-aan ambapo akajibu:

“Hatutaki wawe Dervish.”[1]

Wao wanachojali tu ni siasa. Hawajali elimu, tabia au mambo mengine.

Inapokuja katika Fiqh, wanaruhusu mwanaume kupeana mikono na mwanamke. Wanamwacha mwanamke awe kiongozi na mwanachama katika mashauriano. Wanawaacha hata makafiri wawe wanachama wa watawala katika mashauriano. Ni pote lililo potevu kwa kiasi ambayo haiwezi kutathminiwa.

Ninashangazwa jinsi baadhi wanaweza kuingiwa na hisia na Hizb-ut-Tahriyr. Ninawanasihi watu wote kujitenga nao mbali kabisa na kutahadharisha nao. Lau tusingeliwapatia udhuru kwa tafsiri zao za kimakosa [Ta´wiyl] basi tungeliwakufurisha. Kwa sababu wanapinga adhabu ya kaburi na kujitokeza kwa ad-Dajjaal na kiongozi wao hataki wafuasi wake wajifunze Qur-aan ili wasiwe Dervish.

[1] Tazama  http://en.wikipedia.org/wiki/Dervish

  • Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Tuhfat-ul-Mujiyb (124)
  • Imechapishwa: 30/08/2020