Swali: Katika baadhi ya miji ya Kiislamu kuna makaburi na yanafanyiwa Twawaaf. Je, ni wajibu kwa waislamu walioko huko kufanya Hijrah?
Jibu: Ni juu yako kufanya lile unaloweza. Ni juu yako kuwalingania na kuwabainishia. Ikiwa una elimu wabainishie kuwa ni Shirki na kwamba haijuzu kwa dalili kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Ikiwa huna elimu waelekeze kwa wanachuoni ambao wanaweza kuwabainishia na kuwaelekeza. Fanya lile unaloweza. Allaah (Ta´ala) amesema:
فَاتَّقُوا اللَّـهَ مَا اسْتَطَعْتُمْ
“Basi mcheni Allaah muwezavyo.” (64:16)
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://subulsalam.com/play.php?catsmktba=11649
- Imechapishwa: 01/05/2015
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)