Swali: Ndugu wengi wanapoambiwa jambo fulani ni Bid´ah wanapinga kwa kusema kuwa ni mambo mepesi na kwamba tuangalie yaliyo makubwa zaidi. Unasemaje?

Jibu: Ukweli ni kwamba baadhi ya watu, kama vile al-Ikhwaan al-Muslimuun na Shiy´ah, ambao Uislamu kwa mujibu wao ni kuwapenda na kuchupa mipaka kwa watu wa familia ya kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).

al-Ikhwaan al-Muslimuun wao Uislamu kwa mujibu wao ni al-Haakimiyyah na baadhi ya vijana wa leo. al-Haakimiyyah ni sehemu katika dini. Kuwapenda watu wa familia ya kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ni sehemu katika dini. Madhara ya Bid´ah ni makubwa. Sufyaan ath-Thawriy amesema:

“Bid´ah ni zenye madhara zaidi kwa muislamu kuliko maasi.”

Mzushi anafikiri anafuata uongofu na kwa asilimia kubwa anakufa juu ya Bid´ah yake. Mtenda dhambi kuwa anatenda dhambi na hivyo kunatarajiwa kwake kutubia. Tunamnasihi kufuata Uislamu kikamilifu. Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا ادْخُلُوا فِي السِّلْمِ كَافَّةً

“Enyi mlioamini! Jisalimisheni kikamilifu.”[1]

Madai ya wakomunisti juu ya madaraka ni maovu yasiyotakiwa kukubaliwa. Yale yanayopatilizwa na Suufiyyah na kutikisa vichwa vyao na kubaki juu ya Bid´ah zao. Vivyo hivyo Shiy´ah wao ndio wanaowafungulia njia wakomunisti. Iwapo tutatokea vita kati ya waislamu na wakomunisti basi Shiy´ah wangeliwatumia wakomunisti ili kuwapiga vita waislamu.

[1] 02:208

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 327-328
  • Imechapishwa: 30/04/2025