Swali: Je, wudhuu´ unachenguka ikiwa umemalizika muda wa kupaka juu ya soksi?

Jibu: Ndiyo, unachenguka kwa mujibu wa wanazuoni wengi. Baada ya muda kuisha mtu anapaswa kuvua na kutawadha tena, kwa sababu twahara imeisha.

Swali: Ni ipi dalili, ee Shaykh?

Jibu: Dalili ni muda maalum uliowekwa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam)[1].

[1] at-Tirmidhiy (96), an-Nasaa´iy (127) na Ibn Maajah (478).

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24735/هل-ينتقض-الوضوء-اذا-انتهت-مدة-المسح
  • Imechapishwa: 04/12/2024