Swali: Imepokelewa katika baadhi ya matamshi:

“Hakuna kitu (شخص) kilicho na wivu zaidi kuliko Allaah.”[1]

Jibu: Yote ni sawa. Hakuna kitu au hakuna yeyote. Matamshi yote haya maana yake ni sahihi. Yeye ni kitu, Mtukufu, Yeye ndiye mmoja Mtukufu, Yeye ndiye kitu kitukufu zaidi. Hafananishwi na vitu vingine wala:

لَيْسَ كَمِثْلِهِ شَيْءٌ ۖوَهُوَ السَّمِيعُ الْبَصِيرُ

“Hakuna chochote kinachofanana Naye – Naye ni Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote.”[2]

[1] https://firqatunnajia.com/09-dalili-ya-kwamba-allaah-ni-shakhsw-kitu/

[2] 42:11

  • Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23909/هل-صح-بالحديث-لا-شخص-اغير-من-الله
  • Imechapishwa: 30/05/2024