Haitoshi kutamka shahaadah peke yake

Swali: Ni vipi tutamraddi mwenye kutumia dalili kwa Hadiyth ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu mwenye kusema ”hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah… ” na kwamba kinachotakikana ni kutamka tu na si kufanyia kazi yale inayopelekea…

Jibu: Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakusema atamke tu, amesema:

“Yeyote atakayesema ”hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah hali ya kuwa ni mtakasifu moyoni mwake, ataingia Peponi”.”

“Yeyote atakayesema ”hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah” na akakufuru na vile vinavyoabudiwa badala ya Allaah… ”.”

”Moto umeharamishwa kwa ambaye atasema ”hapana mungu wa haki isipokuwa Allaah” hali ya kuwa anatafuta kwa hilo uso wa Allaah.”

Lazima sharti hili. Shahaadah ina vigezo vyake. Usichukue Hadiyth moja na ukaacha Hadiyth nyenginezo.

  • Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: ad-Durr an-Nadhwiyd (01)
  • Imechapishwa: 06/03/2025