Swali: Je, imethibiti kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alizaliwa tarehe 12 Rabiy´ al-Awwaal? Ni ipi hukumu ya kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake?
Jibu: Haijuzu kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake. Alizaliwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) Rabiy´ al-Awwaal. Lakini haifai kusherehekea siku ya kuzaliwa kwake. Hii ni Bid´ah. Kila Bid´ah ni upotevu. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Tahadharini na mambo yaliyozuliwa. Kwani hakika kilichozuliwa ni Bid´ah, kila Bid´ah ni upotevu na kila Bid´ah ni Motoni.”
Haijuzu kusherekea kuzaliwa kwa Mtume wala kuzaliwa kwa mwengine yeyote.
Usile chakula kilichotengenezwa kwa ajili ya maulidi. Chakula kilichotengenezwa kwa mnasaba wa maulidi usikile.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (98) https://www.alfawzan.af.org.sa/ar/node/18006
- Imechapishwa: 15/05/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket