Gharama za maandalizi ya maiti yanatolewa katika mali yake

Swali: Je, inajuzu kwangu kwa mujibu wa Shari´ah kufanya maandalizi ya mahitaji ya mazishi kwa niaba ya mke wangu, kama mazishi, sanda na mengineyo?

Jibu: Gharama za maandalizi yatolewe kutoka katika mali yake. Ikiwa anayo mali, basi kutoka katika mali yake. Ikiwa hana mali, basi ni juu ya warithi wake, wewe na warithi wengine. Watatekeleza yale yanayohitajika katika maandalizi, sanda, kumuosha, kuchimba kaburi na mambo yanayofanana na hayo. Ikiwa anayo mali yake, basi maandalizi yake kutoka katika mali yake hutangulizwa kuliko warithi.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/1236/حكم-من-قام-بتجهيز-لوازم-دفن-زوجته
  • Imechapishwa: 13/02/2026