Du´aa ambayo haikuthibiti kumuombea maiti

Swali: Mtu akiwa hajui vyema du´aa iliyothibiti ya kumuombea maiti atosheke na kumuombea msamaha tu?

Jibu: Ndio. Atosheke na yale anayoyajua. Hakuna yeyote asiyejua kumfanyia istighfaar maiti na kumuombea rehema. Kila mmoja anayajua haya. Amuombee kwa Allaah rehema, msamaha na kukingwa na Moto kama vile anavyojiombea nafsi yake.

  • Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Sharh ´Umdat-il-Fiqh (15) https://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/Umdah-24-11-1434_0.mp3
  • Imechapishwa: 16/08/2019