Swali 658: Je, inajuzu kuomba kwa du´aa ya ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh):
اللهم إن كنت كتبتني شقيًا فامحه، واكتبني سعيدًا
“Ee Allaah, ikiwa umeniandika miongoni mwa watu waliopotea ifute na uniandike miongoni mwa watu wa furaha”?[1]
Jibu: Dhahiri yake ni kuwa haifa. Bora ni kutofanya hivo.
[1] Ameipokea Ibn Jariyr katika ”Tafsiyr” yake (13/563) kuhusiana na Aayah ya ar-Ra´d:
يَمْحُو اللَّـهُ مَا يَشَاءُ وَيُثْبِتُ ۖ وَعِندَهُ أُمُّ الْكِتَابِ
“Allaah anafuta yale ayatakayo na anathibitisha na Kwake ndiko kuna Mama wa Kitabu.” (39:11)
kupitia kwa Abu Hakiymah, kutoka kwa Abu ´Uthmaan an-Nahdiy, kutoka kwake. Cheni yake ya wapokezi haina neno. Abu Haatim amesema kuhusu Abu Hakiymah katika ”al-Jarh” (7/20):
”Hadhi yake ni ya kuaminika.”
Vilevile tazama ”Tabswir-ul-Muntabiyhiy” (1/405) na ”al-Istighnaa´” cha Ibn ´Abdil-Barr (1/589). Imepokelewa pia riwaya mfano wa hiyo kutoka kwa Ibn Mas’uud.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Masaa-il-ul-Imaam Ibn Baaz, uk. 239
- Imechapishwa: 21/06/2025
- Mkusanyaji: Shaykh Abiy Muhammad ´Abdullaah bin Maaniy´
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket