Dhuhr nyuma ya imamu anayeswali ´Aswr

 Swali: Je, swalah ni sahihi ya ambaye anaswali Dhuhr nyuma ya anayeswali ´Aswr?

Jibu: Hapana vibaya. Swalah yake ni sahihi kwa mujibu wa maoni yenye nguvu. Kwa sababu Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

”Hakika si vyenginevyo kila kitendo kinalipwa kutegemea na nia na kila mmoja atalipwa kutokana na vile alivyonuia.”[1]

Hakukuthibiti kitu kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kinachofahamisha kuwa ni lazima nia ya imamu na maamuma ziendane sambamba. Kwa hivyo kila mmoja analipwa kutegemea na nia yake, kama inavyojulisha Hadiyth hii:

“… na kila mmoja atalipwa kutokana na vile alivyonuia.”

[1] al-Bukhaariy (1) na Muslim (1907).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (12/445)
  • Imechapishwa: 19/04/2026