Swali: Je, inajuzu kwa mwanamke mwenye hedhi kugusa msahafu na kusoma ndani yake?
Jibu: Sijui kama kuna makatazo yoyote ya kufanya hivi. Ama Kauli Yake (Ta´ala):
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Hawaigusi isipokuwa waliotwahara.” (56:79)
Makusudio ni Malaika, kama Alivyosema (Subhaanahu wa Ta´ala) katika Aayah ya ash-Shu´araa:
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ الشَّيَاطِينُ وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
“Na wala hawakuteremka nayo [Qur-aan hii] mashaytwaan na wala haipasi kwao na wala hawawezi.” (26:210)
Na amesema Imaam Maalik katika “al-Mu´attwah”:
“Kauli Yake (Ta´ala): Inafasiriwa na Aayah ya ´Abasaa:
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ بِأَيْدِي سَفَرَةٍ كِرَامٍ بَرَرَةٍ
“Sivyo katu! Hakika hizi ni Ukumbusho. Basi atakaye akumbuke. [Zimeandikwa] katika swahifa zilizokirimiwa. Zimetukuzwa na zimetwaharishwa. [Zinazobebwa] mikononi mwa waandishi, watukufu na watiifu.” (80:11-16)
Yaani hawakuteremka nayo mashaytwaan, isipokuwa imeteremka na Malaika.
“Mikononi mwa waandishi, watukufu na watiifu.”
nao ni Malaika.
Na amepokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake:
“Ibn ´Abbaas alikuwa haonelei mwenye janaba tu kusoma Qur-aan.”
Hakuna ubaya kwa hili – In Shaa Allaah. Tumebakia na Hadiyth nyingine inayosema:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
Hadiyth hii katika njia zake zote, kuna mtu dhaifu ndani yake naye ni Swaalih bin Hujjiyah. Lakini hata hivyo, tunachukua kama alivyoifasiri Imaam ash-Shawkaaniy katika “Nayl-ul-Awtwaar”: Maana yake ni:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa muislamu.”
Abu Hurayrah kapokea pia kuwa:
“Hakika ya muislamu hajanasiki.”
Hivyo, maana yake ni kuwa haigusi [Qur-aan] isipokuwa muislamu tu. Kwa dalili ya kwamba, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikataza kusafiri na Qur-aan katika ardhi miji ya makafiri.
- Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://olamayemen.net/default_ar.aspx?id=8107
- Imechapishwa: 05/03/2018
Swali: Je, inajuzu kwa mwanamke mwenye hedhi kugusa msahafu na kusoma ndani yake?
Jibu: Sijui kama kuna makatazo yoyote ya kufanya hivi. Ama Kauli Yake (Ta´ala):
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
“Hawaigusi isipokuwa waliotwahara.” (56:79)
Makusudio ni Malaika, kama Alivyosema (Subhaanahu wa Ta´ala) katika Aayah ya ash-Shu´araa:
وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ الشَّيَاطِينُ وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ
“Na wala hawakuteremka nayo [Qur-aan hii] mashaytwaan na wala haipasi kwao na wala hawawezi.” (26:210)
Na amesema Imaam Maalik katika “al-Mu´attwah”:
“Kauli Yake (Ta´ala): Inafasiriwa na Aayah ya ´Abasaa:
كَلَّا إِنَّهَا تَذْكِرَةٌ فَمَن شَاءَ ذَكَرَهُ فِي صُحُفٍ مُّكَرَّمَةٍ مَّرْفُوعَةٍ مُّطَهَّرَةٍ بِأَيْدِي سَفَرَةٍ كِرَامٍ بَرَرَةٍ
“Sivyo katu! Hakika hizi ni Ukumbusho. Basi atakaye akumbuke. [Zimeandikwa] katika swahifa zilizokirimiwa. Zimetukuzwa na zimetwaharishwa. [Zinazobebwa] mikononi mwa waandishi, watukufu na watiifu.” (80:11-16)
Yaani hawakuteremka nayo mashaytwaan, isipokuwa imeteremka na Malaika.
“Mikononi mwa waandishi, watukufu na watiifu.”
nao ni Malaika.
Na amepokea al-Bukhaariy katika “as-Swahiyh” yake:
“Ibn ´Abbaas alikuwa haonelei mwenye janaba tu kusoma Qur-aan.”
Hakuna ubaya kwa hili – In Shaa Allaah. Tumebakia na Hadiyth nyingine inayosema:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa aliye msafi.”
Hadiyth hii katika njia zake zote, kuna mtu dhaifu ndani yake naye ni Swaalih bin Hujjiyah. Lakini hata hivyo, tunachukua kama alivyoifasiri Imaam ash-Shawkaaniy katika “Nayl-ul-Awtwaar”: Maana yake ni:
“Haigusi Qur-aan isipokuwa muislamu.”
Abu Hurayrah kapokea pia kuwa:
“Hakika ya muislamu hajanasiki.”
Hivyo, maana yake ni kuwa haigusi [Qur-aan] isipokuwa muislamu tu. Kwa dalili ya kwamba, Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikataza kusafiri na Qur-aan katika ardhi miji ya makafiri.
Mhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: http://olamayemen.net/default_ar.aspx?id=8107
Imechapishwa: 05/03/2018
https://firqatunnajia.com/dalili-kuwa-mwanamke-mwenye-hedhi-anaruhusiwa-kugusa-msahafu-na-kusoma/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)