Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ الشَّيْطَانِ نَزْغٌ فَاسْتَعِذْ بِاللَّـهِ ۖ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
“Utakapokuchochea uchochezi kutoka kwa shaytwaan, basi omba kinga kwa Allaah. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Mjuzi.”[1]
Sulaymaan bin Swurad amesema:
”Nilikuwa nimekaa pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati ambapo wanaume wawili wakitukanana. Mmoja wao uso wake umekuwa mwekundu na mishipa ya shingo yake ikavimba. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Hakika ninajua neno ambalo akilisema yataondoka hayo anayoyapata. Akisema:
أعوذ بالله من الشيطان الرجيم
”Najikinga kwa Allaah dhidi ya shaytwaan aliyefukuzwa.”
yatamwondokea.”[2]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
´Aṭwiyyah bin ´Urwah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika ghadhabu inatokana na shaytwaan na shaytwaan ameumbwa kutokana na moto. Hakika mambo yalivyo ni kwamba moto huzimwa kwa maji. Basi mmoja wenu anaposhikwa na ghadhabu basi na atawadhe.”[3]
Ameipokea Abu Daawuud.
Abu Dharr ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mmoja wenu anapoghadhibika ilihali amesimama, basi na aketi chini. Ikiwa hasira itaondoka ni sawa. Vinginevyo alale chini.”[4]
[1] 41:36
[2] al-Bukhaariy (3282) na (6048) na Muslim (2610).
[3] Abu Daawuud (4784) na Ahmad (6/168). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “adh-Dhwa´iyfah” (582).
[4] Abu Daawuud (4782). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (4782).
- Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Abiy Bakr bin Qayyim-il-Jawziyyah (afk. 751)
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Waabil as-Swayyib wa Raafi´-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 362
- Imechapishwa: 10/09/2025
Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) amesema:
وَإِمَّا يَنزَغَنَّكَ مِنَ الشَّيْطَانِ نَزْغٌ فَاسْتَعِذْ بِاللَّـهِ ۖ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ
“Utakapokuchochea uchochezi kutoka kwa shaytwaan, basi omba kinga kwa Allaah. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia, Mjuzi.”[1]
Sulaymaan bin Swurad amesema:
”Nilikuwa nimekaa pamoja na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati ambapo wanaume wawili wakitukanana. Mmoja wao uso wake umekuwa mwekundu na mishipa ya shingo yake ikavimba. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akasema: “Hakika ninajua neno ambalo akilisema yataondoka hayo anayoyapata. Akisema:
أعوذ بالله من الشيطان الرجيم
”Najikinga kwa Allaah dhidi ya shaytwaan aliyefukuzwa.”
yatamwondokea.”[2]
Ameipokea al-Bukhaariy na Muslim.
´Aṭwiyyah bin ´Urwah amesimulia kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Hakika ghadhabu inatokana na shaytwaan na shaytwaan ameumbwa kutokana na moto. Hakika mambo yalivyo ni kwamba moto huzimwa kwa maji. Basi mmoja wenu anaposhikwa na ghadhabu basi na atawadhe.”[3]
Ameipokea Abu Daawuud.
Abu Dharr ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Mmoja wenu anapoghadhibika ilihali amesimama, basi na aketi chini. Ikiwa hasira itaondoka ni sawa. Vinginevyo alale chini.”[4]
[1] 41:36
[2] al-Bukhaariy (3282) na (6048) na Muslim (2610).
[3] Abu Daawuud (4784) na Ahmad (6/168). Dhaifu kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “adh-Dhwa´iyfah” (582).
[4] Abu Daawuud (4782). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika “Swahiyh Sunan Abiy Daawuud” (4782).
Muhusika: Imaam Shams-ud-Diyn Muhammad bin Abiy Bakr bin Qayyim-il-Jawziyyah (afk. 751)
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Waabil as-Swayyib wa Raafi´-ul-Kalim at-Twayyib, uk. 362
Imechapishwa: 10/09/2025
https://firqatunnajia.com/cha-kufanya-wakati-unapoghadhibika/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket
