Bid´ah kwa mkazi wa Makkah kufanya ´Umrah?

Swali 31: Ni ipi hukumu kwa mkazi wa Makkah kufanya ´Umrah? Je, ni Bid´ah kama ilivyosemwa?

Jibu: Manneo haya yaliyosemwa na muulizaji wameonelea hivo baadhi ya wanazuoni na wakasema kwamba mkazi wa Makkah hana ´Umrah. Lakini dhahiri ya dalili iko kinyume na hilo. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema alipoweka vituo:

”Hizo ni kwa ajili yao na kwa ajili ya yule anayepita kupitia huko kutoka wasio wakazi wake kwa yule anayekusudia Hajj au ´Umrah. Yule aliyeko karibu zaidi na hilo, basi kutoka pale alipoanzia, mpaka watu wa Makkah kutoka Makkah.”[1]

Hii inafahamisha kwamba ´Umrah inaweza kuwa kwa watu wa Makkah. Lakini ikiwa wanataka kufanya ´Umrah, basi ni lazima watoke kwenda Tan´iym au sehemu nyingine ya nje ya Makkah ili waingie ndani ya Ihraam kutoka huko. Allaah ndiye Mjuzi zaidi.

[1] al-Bukhaariy (1526) na Muslim (1181).

  • Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (21/36-37)
  • Imechapishwa: 08/05/2026