Swali: Ni ipi hukumu ya mwanaume anayezini na msichana wake ilihali amelewa?
Jibu: Anatakiwa kuadhibiwa. Kuhusu kusimamishiwa adhabu kwa mujibu wa Shari´ah hapana. Hana adhabu kwa mujibu wa Shari´ah ikiwa amelewa kutokana na maoni sahihi zaidi ya wanazuoni. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
“Allaah amenisamehe ummah wangu kwa ajili yangu makosa, usahaulifu na yale wanayotenzwa nguvu kwayo.”
“Kalamu imenyanyuliwa kwa watu aina tatu; aliyelala mpaka anapoamka, mtoto mpaka anapobaleghe na mwendawazimu mpaka anapopata akili.”[1]
Miongoni mwao akataja mwendawazimu mpaka apate tena akili. Huyu yuko katika hukumu ya wendawazimu. Bakora ziwe za wastani; isiwe kubwa kiasi cha kwamba ukavunja mfupa, na usiwe mdogo kiasi cha kwamba hauumizi. Allaah (Ta´ala) amesema:
وَلْيَشْهَدْ عَذَابَهُمَا طَائِفَةٌ مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ
”Washuhudie adhabu yao kundi la waumini.”[2]
Anatakiwa kupigwa kipigo cha wastani. Asipigwe kwa nguvu sana. Muhimu aadhibiwe.
[1] Abu Daawuud (4405) na Ahmad (1362). Swahiyh kwa mujibu wa al-Albaaniy katika ”al-Irwaa’” (2/5).
[2] 24:02
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 256
- Imechapishwa: 02/04/2025
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket