Baadhi ya vitabu bora na vyepesi kabisa vya ´Aqiydah

Miongoni mwa vitabu vyepesi na bora vya ´Aqiydah ni ”as-Sunnah” cha Ibn Abiy ´Aaswim, ambacho Shaykh Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy (Hafidhahu Allaah) amekifanyia takhriji na kukihakiki, ”as-Sunnah” cha ´Abdullaah bin Ahmad bin Hanbal, ”al-Asmaa’ was-Swifaat” cha al-Bayhaqiy, ”Kitaab-ut-Tawhiyd” cha Ibn Khuzaymah, ”Kitaab-ul-Iymaan cha Ibn Mandah na ”at-Twahaawiyyah”. Ikiwa mtu anaweza kusoma vile vitabu vilivyotangulia, ndio vyepesi zaidi. Pengine ndani yake akapata chembechembe za Kullaabiyyah, Ashaa´irah, Mariysiyyah na wengineo na hivyo ikawa vigumu kwake. Lakini vitabu vya wale waliotangulia ambavyo, ambacho havikuchafuliwa na elimu ya falsafa, ni vyepesi. Vitabu vingine vyenye thamani kubwa ni ”ash-Shariy´ah” cha al-Aajurriy, ”ar-Radd ´alaal-Jahmiyyah”, ”Khalqu Af´aal-il-´Ibaad” na ”Sharh Usuwl I´tiqaad Ahl-is-Sunnah wal-Jamaa´ah” cha al-Laalakaa’iy.

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 500
  • Imechapishwa: 16/07/2025