Baada ya miaka kadhaa wamegundua kuwa msikiti haukuwa ukielekea Qiblah

Swali: Msikiti wa kijiji chetu, baada ya kuswali humo kwa muda fulani, tuligundua baadaye kuwa umeelekea kinyume kidogo na Qiblah. Je, ni lazima turudie swalah zilizopita?

Jibu: Hamna wajibu wa kurudia. Mkengeuko mdogo unasamehewa, na si lazima kurudia swalah. Ikiwa mlibaini kuwa mkengeuko ni mdogo, basi ni vizuri kwa tahadhari kuurekebisha. Lakini ikiwa mkengeuko ni mkubwa, basi ni lazima kuurekebisha na hilo ni jambo haliwezi kujificha. Ama mkengeuko mdogo ndio unaoweza kufichika, nao unasamehewa.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (29/215)
  • Imechapishwa: 26/02/2026