Anayetufu kwenye kaburi ni mshirikina?

Swali: Je, haipelekei kwamba anayetufu anakuwa mshirikina?

Jibu: Ikiwa anakusudia kujikurubisha kwa Allaah, basi hiyo ni Bid´ah. Lakini wengi wa hawa wanaotufu wanajikurubisha kwa makaburi. Hiyo ndio hali yao mara nyingi. Lakini kama akitufu na kusema kwamba anajikurubisha kwa Allaah, basi hiyo ni Bid´ah na ni njia inayopelekea katika shirki kwa yule aliyezikwa ndani ya kaburi.

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31103/ما-حكم-من-يطوف-بالقبور
  • Imechapishwa: 02/10/2025