Anayemwambia ndugu yake `Ee kafiri´ anaritadi?

Swali: Je, mtu huyo anaritadi katika dini?

Jibu: Ni kwa njia ya makemeo na matahadharisho. Haina maana kwamba ameritadi katika Uislamu. Maana yake ni kwamba anastahiki kusifiwa kwa neno hilo[1]. Kwa hivyo ajihadhari kusema hivo. Haina maana kwamba amekufuru na kuritadi katika Uislamu. Hapana sivyo. Maana yake ni kwamba ameingia jambo la khatari ambalo ni baya kwake.

[1] Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:

“Mtu akimwambia nduguye “Ee kafiri!”, basi ni lazima impate mmoja wao.” (Maalik (3/148), Ahmad (2/113), al-Bukhaariy (10/428), Muslim (60) na at-Tirmidhiy (2637)).

  • Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/24165/معنى-اذا-قال-يا-كافر-فقد-باء-به-احدهما
  • Imechapishwa: 11/09/2024