Swali: Anayeficha ushahidi kwa kuchelea juu ya nafsi yake?
Jibu: Allaah anasema:
تَكْتُمُوا الشَّهَادَةَ ۚ وَمَن يَكْتُمْهَا فَإِنَّهُ آثِمٌ قَلْبُهُ
”Msifiche ushahidi; na mwenye kuuficha basi hakika moyo wake ni wenye kutenda dhambi.”[1]
Ni lazima kwake kutekeleza ushahidi. Hata hivyo ikiwa hali inapelekea kwamba anaogopa kuuliwa anapewa udhuru. Lakini ahakikishe – kwa kiasi cha inavowezekana – kuutimiza kwa njia yoyote. Ingawa kwa njia ambayo haitotambulika kuwa si yeye ndiye ametoa ushahidi huo. Hakimu anaweza kusema:
“Nimepewa ushahidi na watu waadilifu au nimepewa ushahidi hivi.”
Ikiwa hakimu anaweza kufanya hivo.
[1] 02:283
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/23927/ما-حكم-من-كتم-الشهادة-خوفا-على-نفسه
- Imechapishwa: 01/06/2024
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket