Swali: Tunaona baadhi ya watu wanapoingia msikitini kwa ajili ya kuswali Fajr na kumeshakimiwa swalah basi wanaswali Rak´ah mbili za Fajr kisha baadaye wanajiunga na imamu. Ni ipi hukumu ya hilo? Je, bora mtu aiswali moja kwa moja baada ya Fajr au asubiri mpaka lichomoke jua?
Jibu: Haijuzu kwa ambaye ameingia msikitini na kumeshakimiwa swalah akaswali Rak´ah mbili za mamkuzi ya msikiti au Raatibah ya msikiti. Bali ni lazima kwake kujiunga pamoja na imamu katika ile swalah inayoswaliwa hivi sasa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Kunapokimiwa swalah basi hapana swalah nyingine isipokuwa ile ya faradhi.”
Ameipokea Muslim katika ”as-Swahiyh” yake.
Hadiyth hii inakusanya swalah ya Fajr na nyinginezo.
Aidha ni mwenye kupewa khiyari; akitaka anaweza kuswali Raatibah baada ya swalah na akitaka anaweza kuichelewesha mpaka baada ya kuchomoza kwa jua na ndio bora zaidi. Kwa sababu imesihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yanayojulisha mambo yote mawili.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/372)
- Imechapishwa: 16/08/2022
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket