Swali: Tunaona baadhi ya watu wanapoingia msikitini kwa ajili ya kuswali Fajr na kumeshakimiwa swalah basi wanaswali Rak´ah mbili za Fajr kisha baadaye wanajiunga na imamu. Ni ipi hukumu ya hilo? Je, bora mtu aiswali moja kwa moja baada ya Fajr au asubiri mpaka lichomoke jua?
Jibu: Haijuzu kwa ambaye ameingia msikitini na kumeshakimiwa swalah akaswali Rak´ah mbili za mamkuzi ya msikiti au Raatibah ya msikiti. Bali ni lazima kwake kujiunga pamoja na imamu katika ile swalah inayoswaliwa hivi sasa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Kunapokimiwa swalah basi hapana swalah nyingine isipokuwa ile ya faradhi.”
Ameipokea Muslim katika ”as-Swahiyh” yake.
Hadiyth hii inakusanya swalah ya Fajr na nyinginezo.
Aidha ni mwenye kupewa khiyari; akitaka anaweza kuswali Raatibah baada ya swalah na akitaka anaweza kuichelewesha mpaka baada ya kuchomoza kwa jua na ndio bora zaidi. Kwa sababu imesihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yanayojulisha mambo yote mawili.
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/372)
- Imechapishwa: 16/08/2022
Swali: Tunaona baadhi ya watu wanapoingia msikitini kwa ajili ya kuswali Fajr na kumeshakimiwa swalah basi wanaswali Rak´ah mbili za Fajr kisha baadaye wanajiunga na imamu. Ni ipi hukumu ya hilo? Je, bora mtu aiswali moja kwa moja baada ya Fajr au asubiri mpaka lichomoke jua?
Jibu: Haijuzu kwa ambaye ameingia msikitini na kumeshakimiwa swalah akaswali Rak´ah mbili za mamkuzi ya msikiti au Raatibah ya msikiti. Bali ni lazima kwake kujiunga pamoja na imamu katika ile swalah inayoswaliwa hivi sasa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Kunapokimiwa swalah basi hapana swalah nyingine isipokuwa ile ya faradhi.”
Ameipokea Muslim katika ”as-Swahiyh” yake.
Hadiyth hii inakusanya swalah ya Fajr na nyinginezo.
Aidha ni mwenye kupewa khiyari; akitaka anaweza kuswali Raatibah baada ya swalah na akitaka anaweza kuichelewesha mpaka baada ya kuchomoza kwa jua na ndio bora zaidi. Kwa sababu imesihi kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) yanayojulisha mambo yote mawili.
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Majmuu´-ul-Fataawaa (11/372)
Imechapishwa: 16/08/2022
https://firqatunnajia.com/anaswali-sunnah-baada-ya-kukimiwa-swalah/