Swali: Ni ipi tafsiri ya maneno Yake Allaah:
يَمْحُو اللَّـهُ مَا يَشَاءُ وَيُثْبِتُ ۖ وَعِندَهُ أُمُّ الْكِتَابِ
“Allaah anafuta yale ayatakayo na anathibitisha na Kwake ndiko kuna Mama wa Kitabu.”[1]
Je, inakusudiwa kwamba anafuta yaliyomo ndani ya Qur-aan au kwenye Ubao uliohifadhiwa?
Jibu: Maana yake ni kwamba Allaah hufuta ayatakayo katika yale aliyoyaweka katika Shari´ah. Anafuta baadhi ya maandiko, kama ilivyotokea kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) alifuta baadhi ya hukumu zilizokuwa Makkah, na kisha Madiynah zikawa tofauti. Mfano ni suala la Qiblah ambapo mwanzoni walikuwa wakielekea Yerusalemu, kisha hukumu hiyo ikafutwa na wakaelekea Ka´bah. Vivyo hivyo yako mambo mengine yaliyotajwa kuwa yamefutwa. Kwa hiyo Allaah hufuta akitakacho. Kadhalika kuna mambo ambayo Yeye (Subhaanah) ameyaning´iniza yanapopatikana ndio hutokea na yasiyopatikana hayatokei. Allaah anafuta ayatakayo na kuyaweka ayatakayo kwa mujibu wa vile ilivyotangulia katika ujuzi Wake na makadirio Yake yaliyotangulia; mambo yote yanarejea Kwake na wala kubadiliki wala kugeuzwa kitu.
[1] 13:39
- Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31009/ما-تفسير-قوله-تعالى-يمحو-الله-ما-يشاء-ويثبت
- Imechapishwa: 21/09/2025
Swali: Ni ipi tafsiri ya maneno Yake Allaah:
يَمْحُو اللَّـهُ مَا يَشَاءُ وَيُثْبِتُ ۖ وَعِندَهُ أُمُّ الْكِتَابِ
“Allaah anafuta yale ayatakayo na anathibitisha na Kwake ndiko kuna Mama wa Kitabu.”[1]
Je, inakusudiwa kwamba anafuta yaliyomo ndani ya Qur-aan au kwenye Ubao uliohifadhiwa?
Jibu: Maana yake ni kwamba Allaah hufuta ayatakayo katika yale aliyoyaweka katika Shari´ah. Anafuta baadhi ya maandiko, kama ilivyotokea kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta´ala) alifuta baadhi ya hukumu zilizokuwa Makkah, na kisha Madiynah zikawa tofauti. Mfano ni suala la Qiblah ambapo mwanzoni walikuwa wakielekea Yerusalemu, kisha hukumu hiyo ikafutwa na wakaelekea Ka´bah. Vivyo hivyo yako mambo mengine yaliyotajwa kuwa yamefutwa. Kwa hiyo Allaah hufuta akitakacho. Kadhalika kuna mambo ambayo Yeye (Subhaanah) ameyaning´iniza yanapopatikana ndio hutokea na yasiyopatikana hayatokei. Allaah anafuta ayatakayo na kuyaweka ayatakayo kwa mujibu wa vile ilivyotangulia katika ujuzi Wake na makadirio Yake yaliyotangulia; mambo yote yanarejea Kwake na wala kubadiliki wala kugeuzwa kitu.
[1] 13:39
Muhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/fatwas/31009/ما-تفسير-قوله-تعالى-يمحو-الله-ما-يشاء-ويثبت
Imechapishwa: 21/09/2025
https://firqatunnajia.com/anafuta-akitakacho/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window) Telegram
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window) WhatsApp
- Click to print (Opens in new window) Print
- Click to email a link to a friend (Opens in new window) Email
- Click to share on Facebook (Opens in new window) Facebook
- Click to share on X (Opens in new window) X
- Click to share on Pocket (Opens in new window) Pocket