Swali: Nikitaka kumuiga muadhini katika adhaana ya al-Fajr na akafika katika kauli “as-Swalaatu khayrun minan-Nawm”, aseme hivo hivo au kuna msemo mwingine wa kusema?
Jibu: Hapana, aseme kama anavyosema muadhini na asiseme kinyume isipokuwa wakati wa “Haiyyaa… “ mbili tu. Mbali na hizi mbili aseme kama anavyosema muadhini, bi maana aseme “as-Swalaatu khayrun minan-Nawm” kama alivyosema muadhini. Isipokuwa kwa dalili inayoonesha umaalum. Na hii ndio Fatwa aliyotoa Shaykh Ibn (Raahimahu Allaah) ya kwamba aseme “as-Swalaatu khayrun minan-Nawm” kama alivyosema muadhini kutokana na ujumla wa Hadiyth:
“Aseme kama anavyosema.”
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Zaad-il-Ma´aad (31) http://www.alfawzan.af.org.sa/sites/default/files/mo–1431-10-10.mp3
- Imechapishwa: 15/11/2014
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)