Swali: Inajuzu kwa mume kumkataza mke wake kuwatembelea na kuwatendea wema ndugu zake? Ni manaswara na wanaishi nje ya nchi hii.
Jibu: Asimkataze kuwatembelea ndugu zake hata kama ni manaswara. Yeye kukutana nao ni katika wema. Asimkataze kuwatendea wema wazazi wake:
وَإِن جَاهَدَاكَ عَلَىٰ أَن تُشْرِكَ بِي مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ فَلَا تُطِعْهُمَا ۖوَصَاحِبْهُمَا فِي الدُّنْيَا مَعْرُوفًا
“Lakini wakikung´ang´ania kwamba unishirikishe na ambayo huna elimu nayo, basi usiwatii na tangamana nao kwa wema duniani.” (31:15)
Mzazi kafiri ana haki ya kutendewa wema na mtoto wake muislamu. Hata hivyo asimpende. Amtendee wema na wala asimpende. Anatakiwa kurudisha wema kutokana na juhudi alizotoa kwake, kumlea na kumhudumia.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (68) http://alfawzan.af.org.sa/node/16495
- Imechapishwa: 26/08/2017
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)