Swali: Je, nimtaliki mwanamke ambaye nimemuoa na baadaye nikaja kujua kuwa hapo kitambo aliwahi kuzini?

Jibu: Akijua kuwa bado anaendelea kuzini aachane naye:

وَحُرِّمَ ذَٰلِكَ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ

”Na imeharamishwa hivyo kwa waumini.”[1]

Lakini akijua kuwa amekwishatubu, ana haki ya kubaki naye kama ambavo ana haki ya kumwacha. Si kwamba ni kamba imefungwa shingoni mwako. Allaah ameifanya talaka kwa ajili ya kumpumzisha mtu.

[1] 24:03

  • Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
  • Tarjama: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Qam´-ul-Mu´aanid, uk. 253-254
  • Imechapishwa: 10/03/2025