Swali: Kuna baadhi ya watu wamenialika nije kutoa kalima katika mnasaba wa sherehe ya mazazi ya Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambapo nikaitikia na nikatoa kalima. Je, nina dhambi kwa kufanya hivo au nazingatiwa ni miongoni mwa waliosherehekea pamoja nao?
Jibu: Ukienda kwao, ukawanasihi, ukawatolea kalima ambayo ukawaonya kutokamana na jambo hilo na ukaenda na usishirikiane nao katika yale wanayofanya kwa njia ya kwamba wasiendelee juu ya Bid´ah yao na juu ya kitendo chao, kitendo cha wewe kwenda na kuwanasihi na ukawabainishia kwamba jambo hilo halijuzu, umefanya vizuri.
- Muhusika: ´Allaamah ´Abdul-Muhsin bin Hamad al-´Abbaad
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Bid´at-ul-Mawaalid wa mahabbat-in-Nabiyy http://www.ajurry.com/vb/showthread.php?t=36078
- Imechapishwa: 10/11/2019
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)