Swali: Je, imeshurutishwa kuweka nia katika Swawm ya Naafilah?
Jibu: Imeshurutishwa, kwa dalili ya Hadiyth:’
“Hakika ya kila kitendo kinategemea nia.”
Ama Hadiyth:
“Yule asiyenuia swawm (katika Uislamu), hana swawm.”
Ni Hadiyth dhaifu haikuthibiti kwa Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hata kama imesahihishwa na baadhi ya wanachuoni wetu.
Pia isitumiwe kama dalili Hadiyth ya Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliingia kwa baadhi ya wake zake akasema: “Je mna chakula”? Akaambiwa “Hapana”. Akasema “Basi nimefunga”.
Kwa kuwa alikuwa amenuia kufunga. Vilevile inajuzu kwa aliyefunga funga iliyopendekezwa kula. Kwa hiyo isitumiwe kama dalili kuwa Mtume (swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) aliweka nia wakati ule. Hadiyth:
“Hakika ya kila kitendo kinategemea nia.”
Ni dalili ya kuwa swawm haisihi kukishapita sehemu ya mchana.
- Muhusika: ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: http://muqbil.net/fatwa.php?fatwa_id=1612
- Imechapishwa: 26/08/2020
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)