Watu hawa kwa aina ya Salmaan al-´Awdah, Safar al-Hawaaliy na ´Aaidh al-Qarniy ni Takfiyriyyuun na ambao wanawachochea ´Awwaam dhidi ya nchi. Maneno yao yameandikwa, yamesajiliwa na yanajulikana. Ni wajibu kwao kutubu kwa Allaah. Hata ´Aaidh al-Qarniy ambaye anasema:

Swali na funga utakavyo

Sio kwa msaada wa Swalah na funga Dini inamtambua mwenye kuabudu

Wewe ni mmoja wa watawa wa padiri

We sio katika Dini ya Ahmad.

Baada ya hapo anaamrisha wale wenye kumtii kupambana na watawala na kusema:

“Usifanyie ubakhili damu yako isiyokuwa na hatia.”

Anawaita vijana kuwa ni watumwa wa Imani na wanaume wa nchi kuwa ni watumwa wa ardhi. Ana mfano wa maneno kama hayo.

Kadhalika Salmaan al-´Awdah. Maneno yake katika “Humuum Fataat Multazimah” yanajulikana. Humo anachochea dhidi ya nchi na kuamrisha kufanya uasi. Yote haya yanaenda kinyume na yale ambayo Allaah Aliamrisha kupitia Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Haijuzu kuwaita “wanachuoni”. Si jengine zaidi ya kuwa ni Khawaarij. Tunamuomba Allaah Azitengeneze hali za Waislamu na Awasalimishe na shari ya Khawaarij hawa. Wanaitakia nchi na wananchi shari. Tunamuomba Allaah Awakinge na yale wanayokusudia.

Kuhusiana na Zayd al-Madkhaliy na Rabiy´ bin Haadiy, hata kama watu watasema yakusema juu yao lakini msimamo wao unajulikana. Wamesema haki, wameandika haki na kuamrisha haki. Ni katika wanachuoni ambao wanapigana Jihaad katika njia ya Allaah kwa ajili ya kunyanyua neno la Allaah.

Ikiwa watu hawa wanawaponda basi ni kwa ajili tu Allaah Anataka wachukue madhambi yao, na madhambi ya wenye kufanya hivo yaongezwe na thawabu zao ziongezwe siku ya Qiyaamah.

[Swali kuhusu hali ya Naaswir al-´Umar]

Jibu: Naaswir al-´Umar ni katika wao.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: http://www.sahab.net/forums/index.php?showtopic=143787
  • Imechapishwa: 23/04/2015