Aina za maimamu:
1- Imamu ambaye hali yake imejificha. Huyu ni yule imamu ambaye hajulikani kuwa na Bid´ah na maovu. Kuswali nyuma ya imamu huyu inajuzu kwa makubaliano ya maimamu wote. Sio miongoni mwa masharti ya uimamu maamuma wajue yale ambayo imamu anaamini na kumpa mtihani kwa kumuuliza nini anachoitakidi.
2- Kuswali nyuma ya mtu wa Bid´ah ambaye analingania katika Bid´ah zake na mtenda dhambi ambaye anadhihirisha maasi yake. Kuna wanachuoni waliofafanua na kusema ikiwa analingania katika Bid´ah zake hakuswaliwi nyuma yake. Na ikiwa halinganii katika Bid´ah zake kunaswaliwa nyuma yake. Vilevile inahusiana na mtenda dhambi. Ikiwa anadhihirisha maasi yake hakuswaliwi nyuma yake. Na ikiwa hadhihirishi maasi yake kunaswaliwa nyuma yake. Usawa ni kwamba ni sahihi kuswali nyuma yake kwa sharti isiwe Bid´ah zake zinamfikisha katika kiwango cha kufuru. Kadhalika isiwe ufuska wake unamfikisha katika kiwango cha kufuru.
3- Imamu kafiri. Haisihi kuswali nyuma yake kwa makubaliano. Kwa mfano mwenye kuabudu makaburi ambaye anaomba asiyekuwa Allaah, anachinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah, anatufu kwenye makaburi au anawawekea nadhiri maiti, hakuswaliwi nyuma yake. Kukiswaliwa nyuma yake basi mtu arudi swalah yake, sawa ikiwa utajua hali yake wakati uko unaswali, kabla ya kuanza au baada ya swalah. Inatakiwa kurudi kuswali swalah yako hata kama itakuwa baada ya muda mrefu.
- Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/534-535)
- Imechapishwa: 19/05/2020
Aina za maimamu:
1- Imamu ambaye hali yake imejificha. Huyu ni yule imamu ambaye hajulikani kuwa na Bid´ah na maovu. Kuswali nyuma ya imamu huyu inajuzu kwa makubaliano ya maimamu wote. Sio miongoni mwa masharti ya uimamu maamuma wajue yale ambayo imamu anaamini na kumpa mtihani kwa kumuuliza nini anachoitakidi.
2- Kuswali nyuma ya mtu wa Bid´ah ambaye analingania katika Bid´ah zake na mtenda dhambi ambaye anadhihirisha maasi yake. Kuna wanachuoni waliofafanua na kusema ikiwa analingania katika Bid´ah zake hakuswaliwi nyuma yake. Na ikiwa halinganii katika Bid´ah zake kunaswaliwa nyuma yake. Vilevile inahusiana na mtenda dhambi. Ikiwa anadhihirisha maasi yake hakuswaliwi nyuma yake. Na ikiwa hadhihirishi maasi yake kunaswaliwa nyuma yake. Usawa ni kwamba ni sahihi kuswali nyuma yake kwa sharti isiwe Bid´ah zake zinamfikisha katika kiwango cha kufuru. Kadhalika isiwe ufuska wake unamfikisha katika kiwango cha kufuru.
3- Imamu kafiri. Haisihi kuswali nyuma yake kwa makubaliano. Kwa mfano mwenye kuabudu makaburi ambaye anaomba asiyekuwa Allaah, anachinja kwa ajili ya asiyekuwa Allaah, anatufu kwenye makaburi au anawawekea nadhiri maiti, hakuswaliwi nyuma yake. Kukiswaliwa nyuma yake basi mtu arudi swalah yake, sawa ikiwa utajua hali yake wakati uko unaswali, kabla ya kuanza au baada ya swalah. Inatakiwa kurudi kuswali swalah yako hata kama itakuwa baada ya muda mrefu.
Mhusika: ´Allaamah ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah ar-Raajhiy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Hidaayah ar-Rabbaaniyyah fiy Sharh al-´Aqiydah at-Twahaawiyyah (01/534-535)
Imechapishwa: 19/05/2020
https://firqatunnajia.com/aina-mbalimbali-za-maimamu-na-hukumu-ya-kuswali-nyuma-yao/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)