Unasema kwenye barua yako:

“Allaah amewanufaisha na kuwaongoza wengi kupitia yeye.”

Wamenufaishwa kivipi? Je, ni manufaa kuwa na anasa na shirki kubwa na kuwanyamazia watu wa Bid´ah na makhurafi? Je, ni manufaa kutokataza maovu na badala yake kutendea kazi kanuni iliyounda Hasan al-Bannaa:

“Twashirikiana kwa yale tunayoafikiana na kupeana udhuru kati yetu kwa yale tunayotofautiana.”

Je, haya ndio manufaa kuita katika ukhaliyfah na kuacha kulingania katika Tawhiyd ambayo ndio njia ya Mitume?

Je, ni manufaa kuita katika mapinduzi dhidi ya nchi zilizoko sasa hata kama itakuwa nchi za Kiislamu zinazohukumu kwa Shari´ah ya Allaah na kusimamisha adhabu ya Kiislamu?

Da´wah ya al-Ikhwaan al-Muslimuun imewaharibu vijana na haikuwanufaisha lolote na kuwafisidi pasi na kuwaboresha.

  • Mhusika: ´Allaamah Ahmad bin Yahyaa an-Najmiy
  • Mfasiri: Firqatunnajia.com
  • Marejeo: Radd-ul-Jawaab, uk. 23
  • Imechapishwa: 10/07/2020