Maana ya Bid´ah ni kuvumbua kitu pasi na kuwa na mfano wake hapo kabla. Amesema (Ta´ala):
بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ
“Mwanzilishi wa mbingu na ardhi.”[1]
Bi maana aliyevianzisha pasi na mfano wake hapo kabla. Amesema (Ta´ala):
قُلْ مَا كُنتُ بِدْعًا مِّنَ الرُّسُلِ
“Sema: “Mimi sikuwa jambo jipya lilozuka katika Mitume.”[2]
Bi maana mimi sikuwa wa kwanza kuja na ujumbe kutoka kwa Allaah kwenda kwa waja. Bali wamenitangulia Mitume wengi. Inasemwa “fulani amevumbua uzushi” bi maana ameanzisha njia ambayo hakutanguliwa. Bid´ah zimegawanyika mafungu mawili:
Ya kwanza: Kuvumbua katika mambo ya kawaida. Kama mfano wa kuvumbua uvumbuzi wa kisasa. Haya yanajuzu. Kwa sababu kimsingi katika mambo ya kiada ni uhalali.
Ya pili: Kuvumbua katika dini. Kitendo hichi ni haramu. Kwa sababu kimsingi ni kukomeka. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atakayezua katika amri yetu hii yale yasiyokuwemo atarudishiwa mwenyewe.”[3]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Mwenye kufanya kitendo kisichoafikiana na amri yetu basi atarudishiwa mwenyewe.”[4]
[1] 02:117
[2] 46:09
[3] al-Bukhaariy (2550) na Muslim (1718).
[4] Muslim (4468).
- Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: ´Aqiydat-ut-Tawhiyd, uk. 167-169
- Imechapishwa: 30/06/2020
Maana ya Bid´ah ni kuvumbua kitu pasi na kuwa na mfano wake hapo kabla. Amesema (Ta´ala):
بَدِيعُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ
“Mwanzilishi wa mbingu na ardhi.”[1]
Bi maana aliyevianzisha pasi na mfano wake hapo kabla. Amesema (Ta´ala):
قُلْ مَا كُنتُ بِدْعًا مِّنَ الرُّسُلِ
“Sema: “Mimi sikuwa jambo jipya lilozuka katika Mitume.”[2]
Bi maana mimi sikuwa wa kwanza kuja na ujumbe kutoka kwa Allaah kwenda kwa waja. Bali wamenitangulia Mitume wengi. Inasemwa “fulani amevumbua uzushi” bi maana ameanzisha njia ambayo hakutanguliwa. Bid´ah zimegawanyika mafungu mawili:
Ya kwanza: Kuvumbua katika mambo ya kawaida. Kama mfano wa kuvumbua uvumbuzi wa kisasa. Haya yanajuzu. Kwa sababu kimsingi katika mambo ya kiada ni uhalali.
Ya pili: Kuvumbua katika dini. Kitendo hichi ni haramu. Kwa sababu kimsingi ni kukomeka. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Atakayezua katika amri yetu hii yale yasiyokuwemo atarudishiwa mwenyewe.”[3]
Katika upokezi mwingine imekuja:
“Mwenye kufanya kitendo kisichoafikiana na amri yetu basi atarudishiwa mwenyewe.”[4]
[1] 02:117
[2] 46:09
[3] al-Bukhaariy (2550) na Muslim (1718).
[4] Muslim (4468).
Mhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: ´Aqiydat-ut-Tawhiyd, uk. 167-169
Imechapishwa: 30/06/2020
https://firqatunnajia.com/90-sura-ya-kwanza-maana-ya-bidah/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)