85- Sunnah atoe Tasliym katika jeneza kimyakimya nyepesi. Ni mamoja imamu na wale waliokowa nyuma yake. Hilo ni kutokana na Hadiyth ya Abu Umaamah katika masuala haya kwa tamko:
“Kisha atoe Tasliym kimyakimya nyepesi pale anapomaliza. Sunnah afanye aliyeko nyuma ya imamu mfano wa vile alivofanya imamu wake.”
Inayo shahidi ambayo imenasibishwa kwa Swahabah. Ameipokea al-Bayhaqiy (04/43) kutoka kwa Ibn ´Abbaas kwamba amesema:
“Alikuwa akitoa Tasliym yenye sauti ndogo.”
Cheni ya wapokezi wake ni nzuri.
Kisha ikapokelewa kutoka kwa ´Abdullaah bin ´Umar kwamba amesema.
“Alikuwa anapoliswali janeza basi huleta Tasliym mpaka awasikilizishe walio nyuma yake.”
Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh[1].
[1] Kana kwamba kutofautiana kwa Aathaar hizi mbili ndio maana zikatofautiana kauli za Hanaabilah juu ya masuala haya. Imetajwa katika “al-Inswaaf” (05/523):
“Imesemwa katika “al-Furuu´”: Dhahiri ya maneno ya maswahiba [Hanaabilah] ni kwamba imamu atoe Tasliym kwa sauti. Na dhahiri ya maneno ya Ibn-ul-Jawziy ni kwamba imamu asome kimyakimya. Kisha ikanukuliwa kutoka kwa “al-Madhhab” na “Masbuuk-udh-Dhahab” yanayolenganisha juu ya maneno ya Ibn-ul-Jawziy, na ndilo lenye nguvu zaidi kutokana na Hadiyth ya Abu Umaamah.”
- Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
- Mfasiri: Firqatunnajia.com
- Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz wa Bid´ahaa, uk. 164-165
- Imechapishwa: 08/02/2022
85- Sunnah atoe Tasliym katika jeneza kimyakimya nyepesi. Ni mamoja imamu na wale waliokowa nyuma yake. Hilo ni kutokana na Hadiyth ya Abu Umaamah katika masuala haya kwa tamko:
“Kisha atoe Tasliym kimyakimya nyepesi pale anapomaliza. Sunnah afanye aliyeko nyuma ya imamu mfano wa vile alivofanya imamu wake.”
Inayo shahidi ambayo imenasibishwa kwa Swahabah. Ameipokea al-Bayhaqiy (04/43) kutoka kwa Ibn ´Abbaas kwamba amesema:
“Alikuwa akitoa Tasliym yenye sauti ndogo.”
Cheni ya wapokezi wake ni nzuri.
Kisha ikapokelewa kutoka kwa ´Abdullaah bin ´Umar kwamba amesema.
“Alikuwa anapoliswali janeza basi huleta Tasliym mpaka awasikilizishe walio nyuma yake.”
Cheni ya wapokezi wake ni Swahiyh[1].
[1] Kana kwamba kutofautiana kwa Aathaar hizi mbili ndio maana zikatofautiana kauli za Hanaabilah juu ya masuala haya. Imetajwa katika “al-Inswaaf” (05/523):
“Imesemwa katika “al-Furuu´”: Dhahiri ya maneno ya maswahiba [Hanaabilah] ni kwamba imamu atoe Tasliym kwa sauti. Na dhahiri ya maneno ya Ibn-ul-Jawziy ni kwamba imamu asome kimyakimya. Kisha ikanukuliwa kutoka kwa “al-Madhhab” na “Masbuuk-udh-Dhahab” yanayolenganisha juu ya maneno ya Ibn-ul-Jawziy, na ndilo lenye nguvu zaidi kutokana na Hadiyth ya Abu Umaamah.”
Mhusika: Imaam Muhammad Naaswir-ud-Diyn al-Albaaniy
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: Ahkaam-ul-Janaa-iz wa Bid´ahaa, uk. 164-165
Imechapishwa: 08/02/2022
https://firqatunnajia.com/86-sunnah-ni-kutoa-tasliym-nyepesi-katika-swalah-ya-jeneza/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)