Swali 78: Nyinyi na ndugu zako wanazuoni wa nchini ni Salafiyyuun. Mnawanasihi watawala kwa njia iliyowekwa katika Shari´ah aliyoibainisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hata hivyo kuna watu wanaokulaumuni kwamba hamkemei madhambi yanayofanywa hadharani. Wengine wanakupeni udhuru na kusema kuwa mnashinikizwa na nchi. Unasemaje juu ya hilo?
Jibu: Hapana shaka kuwa watawala ni kama wanadamu wengine wote, hawakukingwa na makosa. Ni wajibu kuwanasihi[1]. Lakini kuwanyanyasa katika vikao na katika mimbari ni usengenyi ulioharamishwa[2]. Dhambi hiyo ni kubwa kuliko ile inayofanywa na watawala, kwa sababu ni usengenyi. Usengenyi huo unapelekea katika mitihani na mfarakano na kuathiri ulinganizi[3]. Ni lazima kuwanasihi kwa njia ya amani na si kwa njia kuwafedhehesha.
[1] Ibn Abiy ´Aaswim amesema:
”Mlango unaozungumzia wananchi wanapaswa kuwanasihi watawala wao. Zayd bin Thaabit (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Moyo wa muislamu hauingiwi na vifundo juu ya mambo matatu: kumtakasia matendo Allaah, kuwanasihi watawala na kulazimiana na mkusanyiko. Kwa sababu du´aa yao inawazunguka wengine wote.” (as-Sunnah (2/502))
al-Albaaniy amesema kuwa cheni ya wapokezi ni Swahiyh.
[2] Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz (Rahimahu Allaah) amesema:
”Ama kuwatukana viongozi juu ya mimbari sio ufumbuzi. Ufumbuzi ni kuwaombea du´aa ya uongofu, kuwafikishwa, kutengemaa kwa nia na kutengemaa kwa wale marafiki. Hii ndio suluhu. Kwa sababu kuwatukana hakuwazidishii kheri yoyote. Kuwatukana sio katika manufaa. Kuwatukana na kuwalaani sio katika Uislamu.” (Fataawaa al-´Ulamaa’ al-Kibaar, uk. 65, ya ´Abdul-Maalik Ramadhwaaniy)
[3] Pia inapelekea wao kutotiiwa, kutosikizwa katika yaliyo mema na kumwagika kwa damu. ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh) aliuliwa kwa sababu ya makemeo ya waziwazi yaliyozuliwa na Khawaarij.
- Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
- Tarjama: Firqatunnajia.com
- Marejeo: al-Ajwibah al-Mufiydah ´an As-ilat-il-Manaahij al-Jadiydah, uk. 195-200
- Imechapishwa: 21/07/2024
- Taaliki: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
Swali 78: Nyinyi na ndugu zako wanazuoni wa nchini ni Salafiyyuun. Mnawanasihi watawala kwa njia iliyowekwa katika Shari´ah aliyoibainisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Hata hivyo kuna watu wanaokulaumuni kwamba hamkemei madhambi yanayofanywa hadharani. Wengine wanakupeni udhuru na kusema kuwa mnashinikizwa na nchi. Unasemaje juu ya hilo?
Jibu: Hapana shaka kuwa watawala ni kama wanadamu wengine wote, hawakukingwa na makosa. Ni wajibu kuwanasihi[1]. Lakini kuwanyanyasa katika vikao na katika mimbari ni usengenyi ulioharamishwa[2]. Dhambi hiyo ni kubwa kuliko ile inayofanywa na watawala, kwa sababu ni usengenyi. Usengenyi huo unapelekea katika mitihani na mfarakano na kuathiri ulinganizi[3]. Ni lazima kuwanasihi kwa njia ya amani na si kwa njia kuwafedhehesha.
[1] Ibn Abiy ´Aaswim amesema:
”Mlango unaozungumzia wananchi wanapaswa kuwanasihi watawala wao. Zayd bin Thaabit (Radhiya Allaahu ´anh) amesimulia kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema:
”Moyo wa muislamu hauingiwi na vifundo juu ya mambo matatu: kumtakasia matendo Allaah, kuwanasihi watawala na kulazimiana na mkusanyiko. Kwa sababu du´aa yao inawazunguka wengine wote.” (as-Sunnah (2/502))
al-Albaaniy amesema kuwa cheni ya wapokezi ni Swahiyh.
[2] Shaykh ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz (Rahimahu Allaah) amesema:
”Ama kuwatukana viongozi juu ya mimbari sio ufumbuzi. Ufumbuzi ni kuwaombea du´aa ya uongofu, kuwafikishwa, kutengemaa kwa nia na kutengemaa kwa wale marafiki. Hii ndio suluhu. Kwa sababu kuwatukana hakuwazidishii kheri yoyote. Kuwatukana sio katika manufaa. Kuwatukana na kuwalaani sio katika Uislamu.” (Fataawaa al-´Ulamaa’ al-Kibaar, uk. 65, ya ´Abdul-Maalik Ramadhwaaniy)
[3] Pia inapelekea wao kutotiiwa, kutosikizwa katika yaliyo mema na kumwagika kwa damu. ´Uthmaan (Radhiya Allaahu ´anh) aliuliwa kwa sababu ya makemeo ya waziwazi yaliyozuliwa na Khawaarij.
Muhusika: Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Ajwibah al-Mufiydah ´an As-ilat-il-Manaahij al-Jadiydah, uk. 195-200
Imechapishwa: 21/07/2024
Taaliki: Shaykh Jamaal bin Furahyaan al-Haarithiy
https://firqatunnajia.com/78-wanazuoni-wanashinikizwa-na-mamlaka/
Mshirikishe mwenzako:
- Click to share on Telegram (Opens in new window)
- Click to share on WhatsApp (Opens in new window)
- Click to print (Opens in new window)
- Click to email a link to a friend (Opens in new window)
- Click to share on Facebook (Opens in new window)
- Click to share on Twitter (Opens in new window)
- Click to share on Pocket (Opens in new window)